MAKALA MAALUM

Mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara unaelekea kuhitimishwa Alhamisi hii, ambapo baadhi ya timu shiriki zimeonyesha ushindani wa kweli huku zingine zikionekana kama washiriki tu na wasindikizaji.
Timu 14 zinashiriki Ligi Kuu msimu huu ambazo ni Azam FC, Yanga, Simba, Coastal Union, Mgambo Shooting, Oljoro JKT, Kagera Sugar na Ashanti United.
Nyingine ni Mtibwa Sugar, Mbeya City, Tanzania Prisons, JKT Ruvu, Ruvu Shooting na Rhino Rangers.
Hizi zifuatazo  zina njaa na fursa ya kutwaa ubingwa
Azam
Iliunza msimu huu kwa kusuasua kwani ilianza kwa kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Mtibwa Sugar, lakini ilibadilika kadri muda ulivyosonga na kuvuna matokeo mazuri yaliyoipaisha juu  katika msimamo wa ligi.
Azam ina fursa ya kutwaa ubingwa msimu huu kutokana na kuwa na kikosi kilichokamilika, pia inamaliza mzunguko wa kwanza ikiwa katika nafasi za juu katika msimamo wa ligi.
Yanga
Haikuwa na wakati mzuri mwanzoni mwa msimu baada ya kuambulia sare mfululizo katika mechi zake tatu, hata hivyo taratibu ilianza kubadilika na mpaka sasa ipo katika nafasi za juu kwenye msimamo wa Ligi.
Inaweza kutetea taji msimu huu kutokana na kuwa na kikosi chenye mchanganyiko wa wachezaji walioiva vizuri kila idara, hailazimiki kuongeza mchezaji wakati wa usajili wa dirisha dogo mwezi Januari.
Simba

Je wako tayari kurejea Somalia?

Umoja wa mataifa hii leo unajitayarisha kuanza utafiti katika kambi mojawapo kubwa ya wakimbizi duniani Daadab kaskazini mwa Kenya kuchunguza ni kiasi gani cha wakimbizi takriban nusu milioni wa kisomali wapo tayari kurudi nchini mwao.
Wiki iliyopita serikali ya Kenya, Somalia pamoja na shirika la UNHCR, zilitia saini makubaliano ya kuwarudisha nyumbani wakimbizi hao.
Mwandishi wa BBC Bashkas Jugosdaaya alizuru kambi ya Daadab

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni