SIMBA SC WAANZA KUJIFUA KESHO BOKO
KIKOSI
cha Simba ya jijini Dar es Salaam kinatarajia kuanza mazoezi kesho
kwenye Uwanja wa Boko Veteran ulioko Boko kwa ajili ya kujiandaa na
msimu ujao wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara imeelezwa.
Akizungumza
na BIN ZUBEIRY leo mjini Dar es Salaam, Kocha Msaidizi wa Simba,
Selemani Matola, amesema kuwa tayari wachezaji wa timu hiyo wameshapewa
taarifa za kuanza kwa mazoezi hayo tayari kunoa makali kwa msimu mpya wa
ligi. Matola amesema kuwa mazoezi yataanzia gym Chang'ombe na jioni yatakuwa uwanjani.
Amesema
kuwa licha ya kuchelewa kuanza maandalizi yake, wanaamini wachezaji
watakuwa kwenye kiwango cha juu kutokana na kila mmoja kufanya mazoezi
binafsi.
"Kabla
mwalimu ( Zdravko Logarusic) hajaondoka, aliwaeleza wachezaji wajitunze
na wawe wanafanya mazoezi ili kujiweka tayari na programu alizoziandaa
za msimu mpya," amesema.
Kikosi hiko kinatarajia kuanza mazoezi chini ya Matola, kutokana na Logarusic, kuchelewa kuwasili nchini kama ilivyotarajiwa.
Habari
za ndani zilizopatikana jana mchana zinasema kwamba Mcroatia huyo
atawasili nchini Alhamisi na Ijumaa ataungana na wachezaji wake
kuendelea na mazoezi.
Simba pia inatarajia kuelekea Afrika Kusini kuweka kambi ya siku 17 na itaondoka nchini Julai 20.
Hata
hivyo katika kambi hiyo huenda ikawakosa nyota wake watano walioko
katika timu ya Taifa (Taifa Stars) ambao wanajiandaa kuikabili Msumbiji.
Nyota hao ni pamoja na Ramadhan Singano 'Messi', Amri Kiemba, Jonas Mkude, Joram Mgeveke na Haroun Chanongo.
![]() |
| Suleiman Matola kulia akiwa na bosi wake, Zdravko Logarusic |
ARUSHA:
- Hali ya
wasiwasi imeendelea kutanda katika Jiji la Arusha baada ya kitu kinachoaminika
kuwa ni bomu kutegwa katika mkahawa mmoja jijini humo.
Walichofanywa Brazil na Ujerumani hiki hapa

Michuano ya kombe la dunia leo imechukua sura nyingine kabisa baada ya mchezo wa kwanza wa nusu fainali kati ya wenyeji Brazil dhidi ya Ujerumani.
Kwenye mchezo uliopigwa kwenye dimba la Belo Horizonte – Ujerumani wameweka historia ya mbili kubwa – kutinga fainali ya 8 ya kombe la dunia – hii ni mara nyingi kuliko timu zote duniani, pili kuifunga Brazil nyumbani kwao ikiwa ni mara ya kwanza kwa Brazil kupoteza mechi ya ushindani kwenye ardhi yao tangu mwaka 1975.
Magoli ya Ujerumani yalifungwa na Muller, Toni Kroos mawili, Sami Khedira, Ander Schurrle nae akafunga mawili huku Oscar akiifungia Brazil goli moja la kufutia machozi katika mechi iliyoishwa kwa ushindi wa 7-1.
Ujerumani sasa anamsubiri mshindi wa kati ya Argentina vs Uholanzi hapo kesho ili kupata kujua mpinzani wake wa fainali itakayopigwa jumapili hii.
Lawama: Wachezaji wa Brazil, kutoka kushoto Fernandinho, Maicon na David Luiz
La kwanza: Thomas Muller akiifungia Ujerumani bao la kwanza
Kipa Julio Cesar akishindwa kuzuia shut la Thomas Muller, huku David Luiz akiangalia
Mvunja rekodi: Miroslav Klose akishangilia baada ya kuibuka mfungaji bora wa kihistoria wa Kombe la Dunia
Klose amevunja rekodi ya gwiji wa Brazil, Ronaldo akifunga mabao mawili leo
Klose akifunga huku kiungo wa Fernandinho akimsindikiza kwa macho
Kroos akiondoka kushangilia baada ya kufunga
Sammy Khedira akiifungia Ujerumani bao la tano
Ujerumani wakipongezana huku, wachezaji wa Brazil wakitawanyika Uwanja wa Mineirao
Beki wa Brazil, David Luiz akienda chini wakati anakabiliana na Miroslav Klose
Sami Khedira akimtoka Luis Gustavo wa Brazil
Beki wa Ujerumani, Mats Hummels akimzuia Fred huku Oscar akiwa tayari kutoa msaada
Beki wa Ujerumani, Jerome Boateng akizinguana na Marcelo wa Brazil
MAN UNITED WAANZA MAZOEZI, WA ‘MKOPO’ BEBE, ANDERSON, ZAHA….WAREJEA!
MANCHESTER
UNITED Jana walianza Mazoezi rasmi kwa ajili ya Ziara ya Kabla Msimu
Mpya ya huko Marekani na Wachezaji kadhaa waliokuwa nje kwa Mkopo Msimu
uliopita wamerejea na kujumuika huko AON Training Complex Jijini
Manchester
Kutokuwepo kwa Meneja mpya, Louis van
Gaal, ambae bado yuko Brazil akiiongoza Netherlands kwenye Kombe la
Dunia, kulikifanya Kikosi hicho kuwa chini ya Meneja Msaidizi Ryan
Giggs.
Wachezaji hao walianza kurudi Klabuni
tangu Ijumaa iliyokwisha kwa ajili ya upimwaji Afya zao na Mazoezi rasmi
kupangwa kuanza Jana Jumatatu.
Miongoni mwa Wachezaji wa Timu ya Kwanza
waliokuwepo hiyo Jana ni pamoja na Mchezaji mpya Ander Herrera na kina
Jonny Evans, Michael Carrick, Darren Fletcher, Tom Cleverley na Rafael
Da Silva.
Lakini pia Wachezaji kadhaa waliokuwa nje kwa Mkopo Msimu uliopita walirejea na hao ni kina Bebe, Anderson,
Wilfried Zaha, Angelo Henriquez, Jesse Lingard na Nick Powell.
Wilfried Zaha, Angelo Henriquez, Jesse Lingard na Nick Powell.
Bebe alikuwa huko kwao Ureno na Klabu ya
Paços de Ferreira, Anderson alikuwa Italy na Fiorentina huku Angelo
Henriquez, Mchezaji kutoka Chile, alichezea Real Zaragoza.
Msimu uliopita Wilfried Zaha alikuwa Cardiff City, Jesse Lingard alikuwepo Brighton na Nick Powell kuichezea Wigan Athletics.
Wiki hii, Ryan Giggs anatarajiwa kukutana na kila Mchezaji na kuongea nao ana kwa ana.
Wachezaji wengine ambao wamechelewa
kujiunga wenzao ni wale waliokuwepo huko Brazil na Timu zao za Taifa
kwenye Fainali za Kombe la Dunia lakini baadhi yao wanatarajiwa wote
kuwepo kwenye Ziara ya Mareakani.
Hao ni pamoja na Shinji Kagawa, aliekuwa
na Japan huko Brazil, David De Gea, aliekuwa na Spain na Wachezaji wa
England ambao ni Wayne Rooney, Chris Smalling, Phil Jones, Danny Welbeck
na Mchezaji mpya Luke Shaw.
Man United wataruka hapo Julai 18
kuelekea huko Marekani na kupiga Kambi huko California kabla ya kucheza
Mechi yao ya Kwanza huko USA hapo Julai 23 dhidi ya LA Galaxy kugombea
Chevrolet Cup ndani ya Rose Bowl, Pasadena.
USA-ZIARA YA KABLA MSIMU MPYA:
[Zote Nchini Marekani]
Manchester United v LA Galaxy
Chevrolet FC Cup
Jumatano 23 Julai 2014, Rose Bowl, Pasadena
Manchester United v AS Roma
International Champions Cup
Jumamosi 26 Julai 2014, Sports Authority Field, Denver
Manchester United v Inter Milan
International Champions Cup
Jumanne 29 Julai 2014, FedEx Field, Washington DC
Manchester United v Real Madrid
International Champions Cup
Jumamosi 2 Agosti 2014, Michigan Stadium, Ann Arbor





