Jumatano, 9 Julai 2014

SIMBA SC WAANZA KUJIFUA KESHO BOKO


KIKOSI cha Simba ya jijini Dar es Salaam kinatarajia kuanza mazoezi kesho kwenye Uwanja wa Boko Veteran ulioko Boko kwa ajili ya kujiandaa na msimu ujao wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara imeelezwa. Akizungumza na BIN ZUBEIRY leo mjini Dar es Salaam, Kocha Msaidizi wa Simba, Selemani Matola, amesema kuwa tayari wachezaji wa timu hiyo wameshapewa taarifa za kuanza kwa mazoezi hayo tayari kunoa makali kwa msimu mpya wa ligi. Matola amesema kuwa mazoezi yataanzia gym Chang'ombe na jioni yatakuwa uwanjani.
Suleiman Matola kulia akiwa na bosi wake, Zdravko Logarusic 
Amesema kuwa licha ya kuchelewa kuanza maandalizi yake, wanaamini wachezaji watakuwa kwenye kiwango cha juu kutokana na kila mmoja kufanya mazoezi binafsi. "Kabla mwalimu ( Zdravko Logarusic) hajaondoka, aliwaeleza wachezaji wajitunze na wawe wanafanya mazoezi ili kujiweka tayari na programu alizoziandaa za msimu mpya," amesema. Kikosi hiko kinatarajia kuanza mazoezi chini ya Matola, kutokana na Logarusic, kuchelewa kuwasili nchini kama ilivyotarajiwa. Habari za ndani zilizopatikana jana mchana zinasema kwamba Mcroatia huyo atawasili nchini Alhamisi na Ijumaa ataungana na wachezaji wake kuendelea na mazoezi. Simba pia inatarajia kuelekea Afrika Kusini kuweka kambi ya siku 17 na itaondoka nchini Julai 20. Hata hivyo katika kambi hiyo huenda ikawakosa nyota wake watano walioko katika timu ya Taifa (Taifa Stars) ambao wanajiandaa kuikabili Msumbiji. Nyota hao ni pamoja na Ramadhan Singano 'Messi', Amri Kiemba, Jonas Mkude, Joram Mgeveke na Haroun Chanongo.
ARUSHA: - Hali ya wasiwasi imeendelea kutanda katika Jiji la Arusha baada ya kitu kinachoaminika kuwa ni bomu kutegwa katika mkahawa mmoja jijini humo.

Walichofanywa Brazil na Ujerumani hiki hapa

20140709-014045-6045392.jpg
Michuano ya kombe la dunia leo imechukua sura nyingine kabisa baada ya mchezo wa kwanza wa nusu fainali kati ya wenyeji Brazil dhidi ya Ujerumani.
Kwenye mchezo uliopigwa kwenye dimba la Belo Horizonte – Ujerumani wameweka historia ya mbili kubwa – kutinga fainali ya 8 ya kombe la dunia – hii ni mara nyingi kuliko timu zote duniani, pili kuifunga Brazil nyumbani kwao ikiwa ni mara ya kwanza kwa Brazil kupoteza mechi ya ushindani kwenye ardhi yao tangu mwaka 1975.
Magoli ya Ujerumani yalifungwa na Muller, Toni Kroos mawili, Sami Khedira, Ander Schurrle nae akafunga mawili huku Oscar akiifungia Brazil goli moja la kufutia machozi katika mechi iliyoishwa kwa ushindi wa 7-1.
Ujerumani sasa anamsubiri mshindi wa kati ya Argentina vs Uholanzi hapo kesho ili kupata kujua mpinzani wake wa fainali itakayopigwa jumapili hii.

Disbelief: Fernandinho, Maicon and David Luiz look bemused following Germany's fifth goal of the evening
Lawama: Wachezaji wa Brazil, kutoka kushoto Fernandinho, Maicon na David Luiz 
Opener: Thomas Muller scores Germany's first to set Joachim Low's men on their way
La kwanza: Thomas Muller akiifungia Ujerumani bao la kwanza
Back of the net! Goalkeeper Julio Cesar is powerless to stop Thomas Muller's effort as David Luiz watches on
Kipa Julio Cesar akishindwa kuzuia shut la Thomas Muller, huku David Luiz akiangalia
Record-breaker: Miroslav Klose celebrates after becoming the top scorer in World Cup history
Mvunja rekodi: Miroslav Klose akishangilia baada ya kuibuka mfungaji bora wa kihistoria wa Kombe la Dunia
On his knees: Klose broke Brazil legend Ronaldo's goalscoring record as he doubled Germany's advantage
Klose amevunja rekodi ya gwiji wa Brazil, Ronaldo akifunga mabao mawili leo
Lethal finisher! Klose guides the ball into the net as Brazil midfielder Fernandinho watches on
Klose akifunga huku kiungo wa Fernandinho akimsindikiza kwa macho
Kroos-ing to victory: Kroos wheels away to celebrate after scoring his second goal two minutes after his first
Kroos akiondoka kushangilia baada ya kufunga
Easy does it: Sammy Khedira slots the ball home to give Germany into a 5-0 lead on 29 minutes
Sammy Khedira akiifungia Ujerumani bao la tano
Delight and despair: Germany celebrate while Brazil players look on inside the Estadio Mineirao
Ujerumani wakipongezana huku, wachezaji wa Brazil wakitawanyika Uwanja wa Mineirao
Fall to the floor: Brazil defender David Luiz is grounded under the challenge of Miroslav Klose
Beki wa Brazil, David Luiz akienda chini wakati anakabiliana na Miroslav Klose
Midfield battle: Germany's Sami Khedira races forward away from Brazil's Luis Gustavo
Sami Khedira akimtoka Luis Gustavo wa Brazil
Halted: Germany defender Mats Hummels stops striker Fred in his tracks as Oscar looks to retrieve the ball
Beki wa Ujerumani, Mats Hummels akimzuia Fred huku Oscar akiwa tayari kutoa msaada
Little and large: Germany defender Jerome Boateng towers over Brazil left back Marcelo
Beki wa Ujerumani, Jerome Boateng akizinguana na Marcelo wa Brazil

MAN UNITED WAANZA MAZOEZI, WA ‘MKOPO’ BEBE, ANDERSON, ZAHA….WAREJEA!


MAN-UNITED-TOUR2014-LOGO-BESTMANCHESTER UNITED Jana walianza Mazoezi rasmi kwa ajili ya Ziara ya Kabla Msimu Mpya ya huko Marekani na Wachezaji kadhaa waliokuwa nje kwa Mkopo Msimu uliopita wamerejea na kujumuika huko AON Training Complex Jijini Manchester
Kutokuwepo kwa Meneja mpya, Louis van Gaal, ambae bado yuko Brazil akiiongoza Netherlands kwenye Kombe la Dunia, kulikifanya Kikosi hicho kuwa chini ya Meneja Msaidizi Ryan Giggs.
Wachezaji hao walianza kurudi Klabuni tangu Ijumaa iliyokwisha kwa ajili ya upimwaji Afya zao na Mazoezi rasmi kupangwa kuanza Jana Jumatatu.
Miongoni mwa Wachezaji wa Timu ya Kwanza waliokuwepo hiyo Jana ni pamoja na Mchezaji mpya Ander Herrera na kina Jonny Evans, Michael Carrick, Darren Fletcher, Tom Cleverley na Rafael Da Silva.
Lakini pia Wachezaji kadhaa waliokuwa nje kwa Mkopo Msimu uliopita walirejea na hao ni kina Bebe, Anderson, ZAHA-MAN_UNITEDWilfried Zaha, Angelo Henriquez, Jesse Lingard na Nick Powell.ANDERSON
Bebe alikuwa huko kwao Ureno na Klabu ya Paços de Ferreira, Anderson alikuwa Italy na Fiorentina huku Angelo Henriquez, Mchezaji kutoka Chile, alichezea Real Zaragoza.
Msimu uliopita Wilfried Zaha alikuwa Cardiff City, Jesse Lingard alikuwepo Brighton na Nick Powell kuichezea Wigan Athletics.
Wiki hii, Ryan Giggs anatarajiwa kukutana na kila Mchezaji na kuongea nao ana kwa ana.
Wachezaji wengine ambao wamechelewa kujiunga wenzao ni wale waliokuwepo huko Brazil na Timu zao za Taifa kwenye Fainali za Kombe la Dunia lakini baadhi yao wanatarajiwa wote kuwepo kwenye Ziara ya Mareakani.
Hao ni pamoja na Shinji Kagawa, aliekuwa na Japan huko Brazil, David De Gea, aliekuwa na Spain na Wachezaji wa England ambao ni Wayne Rooney, Chris Smalling, Phil Jones, Danny Welbeck na Mchezaji mpya Luke Shaw.
Man United wataruka hapo Julai 18 kuelekea huko Marekani na kupiga Kambi huko California kabla ya kucheza Mechi yao ya Kwanza huko USA hapo Julai 23 dhidi ya LA Galaxy kugombea Chevrolet Cup ndani ya Rose Bowl, Pasadena.
USA-ZIARA YA KABLA MSIMU MPYA:
[Zote Nchini Marekani]
Manchester United v LA Galaxy
Chevrolet FC Cup
Jumatano 23 Julai 2014, Rose Bowl, Pasadena
Manchester United v AS Roma
International Champions Cup
Jumamosi 26 Julai 2014, Sports Authority Field, Denver
Manchester United v Inter Milan
International Champions Cup
Jumanne 29 Julai 2014, FedEx Field, Washington DC
Manchester United v Real Madrid
International Champions Cup
Jumamosi 2 Agosti 2014, Michigan Stadium, Ann Arbor

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni