
Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM chini ya Mwenyekiti wake Rais Jakaya Kikwete, imeanza kuwahoji mawaziri waliotajwa ni ‘mzigo’ kwa Serikali.
Hata hivyo, habari za ndani zilieleza kwamba miongoni mwa ajenda kuu za CC ni kuwahoji mawaziri wanaolalamikiwa na wananchi, kwamba wameshindwa kutekeleza majukumu yao.
Maelfu wakwama kumuaga Mandela

Maelfu ya wananchi wa Afrika Kusini wameshindwa kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Rais wa Kwanza mzalendo wa nchi hiyo, Nelson Mandela kutokana na muda uliopangwa kumalizika.
Kuanzia Jumatano wiki hii hadi jana, mwili wa
Mandela aliyefariki dunia Desemba 4 mwaka huu, ulikuwa ukiwekwa katika
Ikulu ya Pretoria, iliyopo ndani ya Majengo ya Umoja (Union Buildings),
kila asubuhi kwa ajili ya wananchi kutoa heshima za mwisho.
Jana ilikuwa siku ya mwisho ya utoaji wa heshima
hizo na hadi muda uliowekwa ulipokwisha saa 11:30 jioni, kulikuwa na
maelfu ya watu waliokosa fursa ya kumuaga mpendwa wao huyo.
Dalili za idadi kubwa ya watu kukosa nafasi hiyo adhimu zilianza
kuonekana Jumatano na baadaye juzi Alhamisi kwani hadi muda wa kufunga
ulipofika jioni, maelfu ya watu walirejea nyumbani bila kupata fursa ya
kuaga.
Jana mchana, Serikali ilitoa taarifa kwamba kwa
kuzingatia idadi ya watu waliojitokeza kutoa heshima zao za mwisho,
ilikuwa vigumu kwa watu wote kufikiwa.

Abiria 37 waliokuwa wamesafaria ndege ya Shirika la Precision Air, akiwamo Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, jana walinusurika kifo, baada ya magurudumu manne ya ndege hiyo kupasuka ilipokuwa ikitua katika Uwanja wa Ndege wa Arusha.
Lowassa anusurika ajali ya ndege Arusha

Abiria 37 waliokuwa wamesafaria ndege ya Shirika la Precision Air, akiwamo Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, jana walinusurika kifo, baada ya magurudumu manne ya ndege hiyo kupasuka ilipokuwa ikitua katika Uwanja wa Ndege wa Arusha.
Tukio hilo la aina yake, lilitokea saa 6:15
mchana, wakati ndege hiyo, ikitua kutoka jijini Dar es Saalam, ikiwa na
abiria hao 37, marubani wawili na wahudumu wawili.
Kamanda wa polisi mkoani Arusha, Liberatus Sabas alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kueleza hakuna majeruhi aliyeripotiwa.
“Hadi sasa hali ni shwari, ndege iliweza kusimama
licha ya kupasuka magurudumu. Kiutaratibu uchunguzi umeanza kufanywa na
wataalamu husika,”alisema Kamanda Sabas.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni