Jumatano, 4 Desemba 2013

Mamia ya wanahabari nchini Kenya wameandamana nchini humo kupinga sheria mpya ya vyombo vya habari iliyopendekezwa na wabunge na kufanyiwa mageuzi na Rais Uhuru Kenyatta.


Wanahabari hao waliokisiwa kuwa 300 baadhi wakiwa wameziba midomo yao kwa karatasi ya gundi (masking tape) kama ishara ya kukandamizwa, waliwasilisha malalamiko yao kwa bunge la taifa.
Sheria hiyo ambayo bado ni rasimu, itajadiliwa bungeni baada ya Rais kuikataa ilivyoandikwa akiwataka wabunge kuifanyia mabadiliko kabla ya kuifanya sheria.
Wakosoaji wanasema sheria hiyo ikiwa itapitishwa itabana uhuru wa vyombo vya habari licha ya mageuzi yaliyopendekezwa na Rais mwenyewe.
Wanadai kuwa mapendekezo hayo mapya ni makali zaidi kwa uhuru wa vyombo vya habari hata kuliko mapendekezo ya hapo awali yaliyoidhinishwa na bunge kabla ya bwana Kenyatta kukataa kutia saini.

Lissu: Mabadiliko makubwa yanakuja upinzani bungeni

 
Kambi ya Rasmi ya Upinzani Bungeni, itafanya mabadiliko makubwa katika Baraza lake Kivuli wakati wa Mkutano Mkuu wa 14 wa Bunge unaoanza leo mjini Dodoma.
Panga pangua hiyo ambayo imesukumwa na kuvuliwa nyadhifa zote kwa aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chadema na Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Zitto Kabwe itawalenga pia mawaziri vivuli walioshindwa kutimiza majukumu yao kikamilifu.
Habari zilizopatikana jana mjini Dodoma zilisema Zitto ni mlengwa mkuu wa mabadiliko hayo ikiwa ni utekelezaji wa maazimio ya Kamati Kuu (CC) ya chama chake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni