Jumamosi, 10 Agosti 2013

Oprah Winfrey abaguliwa nchini Uswis

Mwanamke maarufu zaidi duniani Oprah Winfrey amekumbana ana kwa ana na kile anachokiita kitendo cha Ubaguzi wa rangi nchini Switzerland baada ya muuza duka mmoja kukataa kumuuzia mkoba wa kike wa mkononi na kumwambia kuwa hangeweza gharama yake.

Oprah ambaye ametajwa katika vitabu vya Forbes kama mwanamke mwenye ushawishi mkubwa wa kisiasa duniani na mmoja wa watu tajiri zaidi amedai kuwa msichana aliyekuwa akiuza hapo dukani alimdharau kutokana na rangi yake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni