Maofisa wa Kikosi Maalumu cha Kupambana na Makosa
ya Jinai na Rushwa cha Afrika Kusini (The Hawks), kiliwakamata watu hao
katika Kitongoji cha Kempton Park, Ekurhuleni, Jimbo la Gauteng.
Msemaji wa Hawks, Paul Ramaloko alisema jana kuwa
maofisa hao walivamia nyumba waliyokuwa wanaishi Watanzania hao na
kukuta mzigo huo. Hata hivyo, alikataa kutaja majina ya watu hao kwa
kuhofia kuharibu uchunguzi akisema bado walikuwa wanawasaka watuhumiwa
zaidi wakiwamo raia wa Afrika Kusini.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni