Zitto alivuliwa uongozi wa Naibu Katibu
Mkuu Taifa na Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, wakati
Dk Mkumbo amevuliwa ujumbe wa Kamati Kuu. Wawili hao wanatuhumiwa
kukisaliti chama.
Taarifa zilisema hoja ya kukisaliti chama pia
ilimkumba Arfi akidaiwa kumwezesha Waziri Mkuu Mizengo Pinda kupita
ubunge bila kupingwa, katika uchaguzi mkuu uliopita na ndiyo sababu ya
kuamua kuachia ngazi nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Taifa.
Mbali ya kuwavua uongozi Zitto na Dk Mkumbo, pia
Kamati Kuu imewapa siku 14 wajieleze kwa nini wasifukuzwe uanachama. Kwa
uamuzi huo Zitto amebaki na wadhifa wa ubunge wake wa Kigoma Kaskazini
na wadhifa mwingine kwenye Kamati ya Bunge.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni