Zitto pamoja na viongozi wengine wawili wa
Chadema; Dk Kitila Mkumbo na Samson Mwigamba walivuliwa nyadhifa zao na
Kamati Kuu ya Chadema baada ya kubainika kupanga mbinu za uasi, kupitia
waraka ambao ulikuwa ukieleza mkakati wa kufanya mabadiliko makubwa ya
kiuongozi wakati wa uchaguzi mkuu wa ndani.
Pinda azitaka Serikali za Mitaa kugawa maeneo ya uwekezaji
Pinda azitaka Serikali za Mitaa kugawa maeneo ya uwekezaji
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amesema, Serikali za Mitaa zikiweza
kujisimamia na kutoa maeneo kwa ajili ya uwekezaji, zinaweza kupiga
hatua za kiuchumi.
Pia amezishauri serikali hizo kuonyesha fursa zilizopo katika uwekezaji kwa lengo la kuwashawishi wawekezaji.
Pinda aliyasema hayo jana wakati akifungua mkutano wa siku mbili wa Ushirikiano wa Serikali za Mitaa kati ya Tanzania na China.
Mkutano huo unawashirikisha wafanyabiashara kutoka
China na Tanzania, magavana na mameya, makuu wa mikoa, wakurugenzi wa
halmashauri za mikoa na wakuu wa wilaya.
Jaji Mkuu aagiza kesi ya Mramba, wenzake iharakishwe
Jaji Mkuu aagiza kesi ya Mramba, wenzake iharakishwe
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande Othman, ameagiza kesi ya matumizi mabaya ya ofisi na kuisababishia Serikali hasara ya Sh11.7bilioni inayowakabili mawaziri wawili wa zamani na katibu mkuu wa zamani wa Wizara ya Fedha, imalizwe haraka.
Mawaziri hao ni Basil Mramba na Daniel Yona na katibu Grey Mgonja, ambao kesi yao iko katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni